Vraiment, les gens manquent de mots à dire pour ce pays. Hier ici à Bunia, on a demandé à un ressortissant du Nord-Kivu de prier à la de prédication, écoutez ce qu’il a dit:
Maombi! Mungu akuwe na tusikia kabisa.
« Mwenyezi Mungu baba yetu, tunakushukuru kwa Neema ya maisha yenye unaendelea tupatia.
Tunasema Sifa na heshima zikurudilie milele na
milele. Tunakuomba utusamehe makosa yetu
yote, kuanzia ku ya ba tate ti ku yetu leo. Baba
utusaidie sana tena sana, ututoshe mu iyi
mateso. Tunateseka sana siye batu beusi, ti
hatujuwe kama tufanye nini. Na tuko najiuliza
kama tulikufanyiaka nini ya mubaya, tulisha
kosa.
Haiko siye peke njoo batoto ya Adamu na Eva
(bazungu, ba chinois, tout comme ba hindi na
baharabu ; siye bote tuko batoto ya Adamu!
Manake, kama ni raha tunapashwa ikula
pamoya, na kama ni mateso, nayo tunapashwa
igabula, isikuwe ya bamoya tu! ).
Baba, hatupashwe endelea teseka ivi juu siye
hatuko mu bale benye baliuwaka mutoto wako
Yesu Kristo. Ni bazungu abo peke njoo
balimuuwaka! Muzungu njoo alimusaliti,
akamutoa ku bengine bazungu. Bale bazungu
bakamubeba ku bengine bazungu benye baka
décider kumutundika ku musalaba. Siye
hatukukuwaka. Yuda Iskarioti, Herode, Caiphe,
Pilato Pontio, Baraba…haziko majina za beusi!
Jina zetu ni Chiribagula, Mushobekwa,
Kahonghya, Bigirimana, Mutombo, Ndushabandi,
Kongolo, Mutanava, Ngalukiye, Masika… Akuna
kabila yetu yenye muko ndani majina sawa
Petro, Iskarioti, Herode, etc. Majina za kwetu
sawa vile Chubaka, Bashibagugumba,
Mudahingwa, Ndoole, Sekimonyo, Nyirabijumba,
Aharerimana, Omalanga, Loboloko,
Mushagalusa, Boboliko, Kyalondawa, Katembo,
Mbachi-Mbacha, Visombwere, …hazikuwake mu
Biblia.
Na zile dini (ao bikundi )za Bafarisayo,
Basadukayo,Bazeloti, etc; siye yetu hatuzijuwe!
Njoo vile Baba, mutoto wako, siye
hatukumufikishaka ako ata kofi moya. Na
mwenye alimukanaka mara tatu hakukuwaka
mweusi! Tungelikuwaka, tungelisemaka
bamuache, juu siye tunakuwaka batu ya uruma
sana. Na bazungu banaoneshaka mu films zabo
gizi abo benyewe njoo baliuwaka Yesu. Ile kilima
ya Golgotha, siye hatujuwe ata kwenye
kinakuwaka. Mu geographie yetu, tunajuwa
comme bilima Kahuzi, Nyiragongo, Nyamulagira,
Ruwenzori, Kilimandjaro… Akuna ata kimoya
mu bile bilima kyenye kinasemekana mu Biblia.
Yerusalemu tulipasikiaka siku muzungu
alituleteaka Biblia. Avant pale, tulikuwaka
hatujuwe ata kama zile mingini zote za mu
Biblia zinakuwaka. Siye tunajuwa tu Kinshasa,Bukavu,
Lubumbashi, Kisangani, Goma, Kigali, Nairobi,
Bangui, Uvira… Mu zile mingini zetu zote
hakuna kwenye Yesu balimupigiaka ata fimbo
moya. Hatukumuchambaka ata ako!
Ile muti yenye ilijengaka musalaba yenye
balimutundikiaka ako, ilitokaka njoo Galilaya
(kule kule tu ku bazungu); haikutokaka mu
forêt Équatoriale (balikuwaka habajuwe ata
kwenye ile forêt inakuwaka ile masiku!).
Misumari zenye balimupigaka, zilikuwaka za ba
Romains (bazungu!), siye tulikuwaka na hatuya
kuwaka na usine ya misumari za vile zile
masiku. Na ule mwizi mwenye alikuchambiaka
mutoto ku musalaba najapo naye anatundikiwa,
naye alikuwaka muzungu.
Oh, baba, ukumbuke alakini gizi mwenye
alisaidiaka mutoto yako kubeba musalaba ni
Africain mwenzetu, ule Simon de Cyrene.
Hatujuwe kama alijifikishaka kule aye wala
kama ni buyuwayi gani njoo aliendaka fanya
kule! Alakini alisaidiaka mutoto wako, na njoo
ya maana ile. Na siku Yesu alikuwaka akingali
bébé, saa Herode alitafutaka muuwa, ni Misri
njoo alikimbiliaka, benzetu beusi bakamuweka!
Kuwa ata natukumbukia ku zile mema mbili
baba; na siye tuko batoto yako! Tusaidie baba,
surtout siye baKongomani. Ututoshe mu iyi
mateso yote. Angalia ata weye peke ma kanisa
za pata zenye tulishaka kujengea! Kila siku
tunakutosheaka nyimbo za mupya, na siye njoo
tunakutumiaka maombi za trop tena za mu kila
sauti. Tusaidie sasa na siye tuwine sawa
bazungu, tu ba coloniser na siye, tukule ku raha
sawa bengine. Hatupashwe teseka ivi najapo
haiko siye njoo tulikuuwiaka wala kukukania
mutoto baba. Kwa jina la Yesu Kristo, Amen! »
Espérons que iyi prière ilifikaka…