Wengi hawakutuamini wakati tuliwakataza kuenda kuchagua wagenyi ku miaka 2006 na 2011. Tshisekedi naye, alidanganyika sana, akifikili kushinda ule adui kwa nguvu yake pekee, bila matayarisho ya kanuni. Leo, inaonekana wazi ya kwamba, bila msaada ya wakongomani yote, atashindwa kabisa.
Leo vile vile, ku inchi yetu ya Kongo, mukongomani anazidi kupigwa, kulumizwa, kuuwa na wapolisi pamoja na waaskari.
Kesho, wengi watakuuwa tena na bunduki, wakipigwa ao na sumu. Tusipokataa kuzidi kutumikia Yusufu Hypolite Kanambe, hakutakuwa kimia hata siku moja ku inchi yetu ya Kongo.
Kwa mapenzi ya Bwana, wakristu wameisha nao kulamuka.
Kanambe na watumwa yake, badae, watashindwa. Alakini mbele ya Kanambe kushindwa, wakongomani wengi watakufa tena ; kwani, hawakupenda wala wengine hawajapenda kusikia sauti ya wapelelezi ya Mungu !
http://www.voxafrica.com/vod/videos/?v=0_dq1z580w
